RAIA WAWILI WA AFRIKA KUSINI NCHINI JAPAN WAPATA CORONA


Watu wawili raia wa Afrika Kusini, wafanyakazi katika meli ya ‘Diamond Princess Cruise Ship’ wamekutwa na virusi vya Corona nchini Japan.

Hii ni kesi ya kwanza ya virusi vya Corona kwa wananchi wa Afrika Kusini ndani na nje ya nchi.

Alhamis Februari 27, rais wa nchi hiyo Cyril Ramaphosa, alitangaza kuwarudisha nyumbani wananchi wote wa Afrika Kusini waliopo Wuhan, China, eneo mlipuko wa virusi hivyo ulipoanzia.

Huku virusi vya Corona vikiendelea kutapakaa sehemu mbalimbali duniani, kwa Afrika Nigeria wiki hii, imerekodi muathirika wa virusi vya Corona ambaye ni raia wa Italia.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527