MSANII MWANA FA AKUTWA NA VIRUSI VYA CORONA...ATOA UJUMBE KWA WATANZANIA


Msanii wa muziki wa Hip Hop hapa nchini Mwana FA, amekutwa na maambukizi ya homa kali inayosababishwa na virusi vya Corona na kwamba amewekwa karantini na kwa sasa anaendelea vizuri.

Kupitia video aliyorekodi Mwana FA ameeleza kuwa siku chache zilizopita alikwenda nchini Afrika Kusini na wakati anarudi alianza kujihisi kuwa na homa kali.


Hali hiyo ilimfanya kwenda hospitali na kutaka apimwe kubaini kama ana corona na majibu yametoka leo yakionyesha kuwa ana ugonjwa huo.
 
"Nilivyorudi nikajitenga ili kuhakikisha siambukizi wengine, ugonjwa huo unaweza ukampata mtu yoyote na homa niliyokuwa nayo juzi haipo tena kwa sasa nipo shwari, tujihadhari tu, COVID-19 si ugonjwa wa kutisha sana, kwa sababu tumekuwa tukipata magonjwa mabishi zaidi ya hii" amesema Mwana FA.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527