Breaking : WAANDISHI WANNE WA HABARI WAUNGUA MOTO MOROGORO



Na Jackline Lolah Minja - Malunde  1 blog
Waandishi wa habari wanne wa Star TV, Global Publishers, Abood Media na Imani Media wameungua baada ya kulipukiwa na mtungi wa gesi, eneo la Mizambarauni Msamvu Morogoro, walipokuwa wakifuatilia taarifa ya moto.



Taarifa za awali zinasema waandishi hao wa habari ni Omary Hussein wa Star TV, Salum  Yusuph wa Abood media, Hassan Ninga wa TV Imaan na Nicko wa Global Publishers wamelazwa hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro kwa ajili ya matibabu matibabu  na wameungua moto baada ya mtungi wa gesi kulipuka wakati wa uokoaji na wao wakiendelea kupiga picha. 

 Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Morogoro (Morogoro Press Club) Nickson Mkilanya amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa waandishi hao wa habari wamekumbwa na tukio wakati wakitekeleza majukumu yao.

 "Nimepokea taarifa za ajali ya moto kwa waandishi hawa habari kwa masikitiko, walikuwa wanawajibika na mpaka sasa waandishi wa habari  wawili ambao ni Omary Hussein na Salum bado wapo hospitali wanaendelea na matibabu. Hassan Ninga na Nicko  wameruhusiwa  kutoka",amesema Mkilanya wakati akizungumza na Malunde 1 blog.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Wilbroad Mutafungwa amesema tukio hilo limetokea leo Jumamosi Majira ya saa nane na nusu mchana.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post