MWANAFUNZI WA CHUO KIKUU AJIUA KWA KUJIRUSHA GHOROFANI CHUONI


Picha ya mahali ambapo mwanafunzi huyo amejirusha

Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mount Kenya,amefariki dunia kwa kujirusha kutoka ghorofa ya saba katika jengo la Chancellors Tower linalomilikiwa na chuo hicho.

Naibu wa Jeshi la Polisi wa Mji wa Nakuru Daniel Kitavi, amesema mwanafunzi huyo amefariki dunia wakati anapatiwa matibabu katika hospitali ya Thika Level V, ambapo alikimbizwa baada ya kujirusha kutoka ghorofani na kwamba aliumia zaidi maeneo ya kichwani.

Aidha wanafunzi wenzake walidai kwamba, mwenzao huyo alikuwa anajitishia kujitoa uhai kwa sababu ya matatizo yake binafsi.

Chanzo : Citizen Digital

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post