![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiZ3pRuGZ4G1cOLYB3k8mw5Qyem1mlESo7NoIYhzb6lElMNcFk0aQS-It_NCxp2KnLZkHnzQDKofQetyJPWY7x2aJRphtZ9Lm-UvlOOGYDmJm8tzlPnPFKIeuJUL_DnW6EOFsL7974IfN_i/s640/1.png)
Serikali ya Kenya imesimamisha safari za ndege kutoka Kaskazini mwa Italia kutokana na mlipuko wa nimonia ya COVID-19 nchini humo.
Mwenyekiti wa Kamati ya kitaifa ya mwitikio wa dharura dhidi ya COVID-19 Bw. Mutahi Kagwe, amesema safari za ndege kutoka Kaskazini mwa Italia, hasa miji ya Verona na Milan, kwenda mkoa wa pwani nchini Kenya zimesimamishwa kuanzia tarehe 3 mwezi Machi.
Bw. Kagwe ambaye pia ni waziri wa afya wa Kenya amesema, Kenya itaendelea kufuatilia hali ya nchini Italia na kurekebisha sera yake kulingana na maendeleo ya hali.