KENYA YASIMAMISHA SAFARI ZA NDEGE KUTOKA KASKAZINI MWA ITALIA


Serikali ya Kenya imesimamisha safari za ndege kutoka Kaskazini mwa Italia kutokana na mlipuko wa nimonia ya COVID-19 nchini humo.

Mwenyekiti wa Kamati ya kitaifa ya mwitikio wa dharura dhidi ya COVID-19 Bw. Mutahi Kagwe, amesema safari za ndege kutoka Kaskazini mwa Italia, hasa miji ya Verona na Milan, kwenda mkoa wa pwani nchini Kenya zimesimamishwa kuanzia tarehe 3 mwezi Machi.

Bw. Kagwe ambaye pia ni waziri wa afya wa Kenya amesema, Kenya itaendelea kufuatilia hali ya nchini Italia na kurekebisha sera yake kulingana na maendeleo ya hali.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post