CHINA YAITAKA MAREKANI IIONDOLEE IRAN VIKWAZO


Marekani haionyeshi uwezekano wa kupunguza vikwazo kwa Iran licha ya ombi kutoka China kwamba ingefanya hivyo kwa sababu ya janga la mlipuko wa virusi vya corona. 

Vyanzo vyenye uzoefu wa mvutano kati ya Marekani na Iran vimesema kuwa utawala wa Trump unaona kwamba Iran bado haitaki kubadilika. 

Vyanzo hivyo vinavyojumuisha maafisa wa Marekani, wanadiplomasia na wachambuzi, wamebainisha kua Marekani iliiwekea Iran vikwazo vipya ili kuishinikiza zaidi kuhusiana na mpango wake huo wa makombora ya nyuklia na pia kuilazimisha iache kuviunga mkono vikosi vya wapiganaji katika nchi za Iraq, Yemen na Lebanon.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527