WAANDISHI WA HABARI WASHAURIWA KUWA WAZALENDO, KUTUMIA VYEMA KALAMU NA MIDOMO YAO KATIKA USTAWI WA TAIFA


Mkurugenzi wa Benki Kuu ya Tanzania Tawi la Arusha, Bw. Charles Yamo, akisoma hotuba ya ufunguzi wa semina kwa waandishi wa habari za uchumi na fedha kwenye ukumbi wa BoT jijini Arusha Machi 2, 2020.
****
WAANDISHI wa habari nchini wameshauriwa kuwa wazalendo kwa taifa kwa kutumia vyema kalamu zao, midomo yao na vyombo vyao vya habari kwa kuhabarisha umma vyema bila kuharibu uelekeo wa ustawi wa taifa.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Arusha wakati akifungua semina kwa wanahabari kuhusiana na habari za Uchumi na Fedha Mkurugenzi wa Benki kuu ya Tanzania (BOT) tawi la Arusha Charles Yamo amesema kuwa umuhimu wa vyombo vya habari katika ujenzi wa taifa ni mkubwa sana hivyo ni lazima Wanahabari wawe chachu ya maendeleo ya Taifa kwa ujumla.

"Kupitia mafunzo haya tunaamini umma utaelewa zaidi ni nini benki kuu inafanya na nini wategemee kutoka kwetu" Ameeleza.

Amesema kuwa kupitia mafunzo hayo wanahabari watapata fursa ya kufahamu zaidi kuhusiana na sera za fedha, masoko ya sekta ya fedha, usimamizi wa fedha na huduma za kibenki na kupitia maarifa hayo wananchi watapata fursa ya kupata elimu zaidi kuhusiana na majukumu yanayotekelezwa na benki kuu ya Tanzania.

Aidha Yamo amewashauri waandishi wa habari kujiendeleza kielimu ili kwenda sambamba na maendeleo ya sayansi na teknolojia.

"Dunia imebadilika teknolojia inakua kwa kasi ni vyema wanahabari mkajiendeleza zaidi kielimu ili kuweza kutayarisha na kuandika habari zitakazowafikia wananchi kwa urahisi zaidi" Ameeleza.

Pia amesema kuwa umahiri kwa wanahabari ni jambo lisiloepukika hivyo ni vyema kwa kila mwanahabari kubobea katika sekta fulani kiuandishi na kuimakinikia.

"Ukiwa na sekta ambayo umeibobea utaitendea vyema kazi yako na sio kuandika kila kitu, ukiwa mahiri na mweledi katika sekta ya uchumi au kilimo itakupa nafasi zaidi ya kuitendea kazi vyema" amesema.

Mafunzo hayo kwa waandishi wa habari yatakwenda sambamba na kutembelea miradi mbalimbali ya kiuchumi inayotekelezwa na Serikali ya awamu ya tano jijini Arusha.

Kwa upande wake Meneja Msaidizi wa Uhusiano na Itifaki, BoT, Bi. Vicky Msina mwanzoni mwa semina hiyo, alieleza kuwa washiriki wa semina hiyo wanatoka kwenye vyombo mbalimbali vya habari vikiwemo vya televisheni, radio, magazeti na mitandao ya kijamii na kwamba semina hiyo itadumu kwa siku tano ambapo wataalamu wa BoT watatoa elimu kuhusu shughuli za BoT.
Mkurugenzi wa Benki Kuu ya Tanzania Tawi la Arusha, Bw. Charles Yamo, akisoma hotuba ya ufunguzi wa semina kwa waandishi wa habari za uchumi na fedha kwenye ukumbi wa BoT jijini Arusha Machi 2, 2020.
Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Tafiti za Uchumi BoT, Dkt. Suleiman Misango, akiendelea kutoa ufafanuzi kuhusu ukuaji wa Uchumi nchini kwenye semina ya Waandishi wa Habari za Uchumi na Fedha inayofanyika jijini Arusha.
Meneja Msaidizi wa Uhusiano na Itifaki BoT, Bi. Vicky Msina (katikati) akitoa maelezo ya awali kuhusiana na semina hiyo. Kushoto ni Mkurugenzi wa BoT tawi la Arusha, Bw. Charles Yamo na kulia ni Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Tafiti za Uchumi BoT, Dkt. Suleiman Misango.
Meneja Msaidizi wa Uhusiano na Itifaki BoT, Bi. Vicky Msina akitoa maelezo ya awali kuhusiana na semina ya Waandishi wa Habari za Uchumi na Fedha inayofanyika jijini Arusha.
Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Tafiti za Uchumi BoT, Dkt. Suleiman Misango, akifafanua moja ya mada iliyohusu mapitio ya maendeleo ya uchumi nchini, kikanda na dunia na matarajio kwa mwaka 2020,Kwenye Semina ya Waandishi wa Habari kutoka vyombo mbalimbali ikiwemo mitandano ya Kijamii iliyohusu Habari za Uchumi na Fedha,inayofanyika jijini Arusha
Wanahabari wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye semina hiyo inayoendelea jijni Arusha
Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Tafiti za Uchumi BoT, Dkt. Suleiman Misango, akitoa mada kuhusu mapitio ya maendeleo ya uchumi nchini, kikanda na Dunia na matarajio kwa mwaka 2020.
Baadhi ya Wanahabari wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa na Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Tafiti za Uchumi BoT, Dkt. Suleiman Misango kuhusu mapitio ya maendeleo ya uchumi nchini, kikanda na dunia na matarajio kwa mwaka 2020.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post