ZITTO KABWE AREJEA TANZANIA


Kiongozi wa Chama cha ACT- Wazalendo Zitto Kabwe amewasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere Jana Jumatatu February 17, 2020 akitokea ziarani katika mataifa mbalimbali ikiwemo Marekani na Uingereza ambapo amesema ziara yake imekuwa ya mafaniko makubwa.


Akizungumza baada ya kuwasili  amedai kuwa bado hana hofu ndio maana amerudi nchini

“Sina hofu na ndio maana nimerudi bila shida yoyote kwa sababu hamna kosa lolote nimefanyana ,nitaendeea kufanya shughuli zangu kama kawaida,.” alisema 

Aidha, Zitto alisema kwa sasa chama chake kiko kwenye mchakato wa uchaguzi na anatafakatri kuwa anachukua fomu ya kugombea nafasi gani ndani ya chama hicho

Hivi karibuni  Zitto Kabwe alitupiwa lawama nyingi na wabunge mbalimbali katika mkutano wa 18 wa Bunge uliomalizika hivi karibuni mjini Dodoma kwa kitendo chake cha kuiandikia barua Benki ya Dunia (WB) akitaka isiidhinishe mkopo wa Sh1.2 trilioni kwa Tanzania kwa ajili ya sekta ya elimu.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527