WAZIRI MKUU AWATAKA WATUMISHI WA UMMA WATENGE MUDA WA KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ametaka watumishi wa umma nchini kote kutenga muda wa kusikiliza kero za wananchi.


Alitoa maagizo hayo jana mjini hapa wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika uwanja wa Mwanga Community Centre, Manispaa ya Kigoma Ujiji.

“Watumishi mnatakiwa kwenda kwa wananchi na kusikiliza kero na kushirikiana nao kuzipatia ufumbuzi. …hamuendi na kama mngekuwa mnaenda kusingekuwepo na mabango kwani kitendo cha kuwepo mabango ni ishara tosha kuwa hamuendi,” alisema.

Alisema Serikali imepeleka fedha nyingi mkoani Kigoma za kugharamia miradi ya maendeleo zikiwemo sh bilioni 4.6 za ununuzi wa dawa ambapo Manispaa ya Kigoma Ujiji inapata sh milioni 50 kila mwezi hivyo hakuna sababu wananchi kukosa dawa.

Alisema Serikali ya Rais Dk John Magufuli imedhamiria kuboresha na kusogeza huduma za afya kwa kujenga vituo vya afya karibu na wananchi zikiwemo za afya ili kuwapunguzia watu, kutembea umbali mrefu hadi hospitali za wilaya au mkoa.

Waziri Mkuu aliuagiza uongozi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji kupitia Baraza la Madiwani kusimamia vizuri matumizi ya fedha zinazotolewa na Serikali ili kugharamia miradi ya maendeleo.

Alikemea wananchi katika maeneo mengi ya mkoa wa Kigoma kudai fidia maeneo hata ya mapori na kukwamisha baadhi ya miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa hospitali ya kanda.

Awali, Waziri Mkuu alishiriki swala ya Ijumaa katika msikiti wa Mujahidina uliopo eneo la Buzebazeba mijini Kigoma.

Alitumia fursa hiyo kuwausia waumini wa dini ya Kiislam na wananchi kwa ujumla kuendelea kushikamana na kulinda amani. Pia aliwahamasisha walime zao la michikichi


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527