K-LYINN ADAI KUZUIWA KUINGIA KWENYE KABURI LA REGINALD MENGI


Takriban mwaka mmoja baada ya kifo cha bilionea wa Tanzania Reginald Mangi, tayari kumeibuka mgogoro katika familia yake, baada ya mkewe Jacqueline Mengi kudai kwamba amenyimwa kuona kaburi la mumewe.


Katika chapisho lake la twitter, Klynn kama anavyofahamika anasema kwamba amenyamaza vyakutosha. Na sasa ameshindwa kuvumilia baada ya yeye na wanawe pacha kuzuiwa kuona kaburi hilo na kwamba walihitaji kuomba ruhusa.

Katika chapisho hilo malkia huyo wa urembo wa zamani anaendelea kusema kwamb; "Mmefikia hatua ya kunizuia mimi na wanangu kuingia kwenye kaburi la mume wangu, tunafukuzwa eti mpaka tuombe ruhusa ya kuingia kwenye kaburi la mume na baba wa watoto wangu! Nimechoka , sitakubali kuendelea kuona wanangu wakisononeka na sitakaa kimya", alisema Klynn.

Reginald Mengi alifariki mwaka jana mwezi Mei tarehe 2 huko Dubai akiwa na umri wa miaka 75. Wawili hao walikuwa wamefunga ndoa mwaka 2015 na kupata watoto wawili.

Familia ya bilionea huyo haijatoa tamko lolote.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527