VIKOSI VYA SYRIA VYAENDELEA KUSONGA MBELE....VYATEKA SEHEMU KUBWA YA MKOA WA ALEPPO


Vyombo vya habari nchini Syria vinasema vikosi vya serikali vimepiga hatua muhimu na kuyateka maeneo mengi yaliyokuwa chini ya udhibiti wa waasi katika mkoa wa Aleppo ulioko kaskazini magharibi mwa nchi hiyo. 

Mafanikio haya ya serikali yametangazwa siku moja kabla mazungumzo mapya kati ya Urusi na Uturuki kuhusiana na kuongezeka kwa mapigano katika eneo hilo. 

Hatua hii ya serikali ya Syria imeutatiza ushirikiano kati ya Uturuki na Urusi, ambazo wanaunga mkono pande tofauti katika mzozo huo wa miaka tisa, ingawa zinashirikiana katika kutafuta suluhisho la kisiasa. 

Kulingana na wanaharakati, hapo jana ndege za kivita za Urusi ziliishambulia miji kadhaa ukiwemo wa Anadan ambao baadaye ulitekwa na vikosi vya Syria vinavyoungwa mkono na wanamgambo wa Iran. 

Duru za kijeshi zimearifu kwamba wapiganaji wa upinzani wameondoka kutoka Anadan na mji wa Haritan.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527