MAKONDA AGOMA KUZUNGUMZIA KUZUIWA KUINGIA NCHINI MAREKANI

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amegoma  kuzungumzia kuzuiwa kuingia nchini Marekani kwa maelezo kuwa kuna siku atalizungumzia suala hilo.


Makonda ametoa majibu hayo leo Ijumaa Februari 14, 2020 wakati akihojiwa katika kipindi cha 360 kinachorushwa na televisheni ya Clouds

Katika kipindi hicho ambacho Makonda alikuwa anazungumzia mambo mbalimbali  ya mkoa wa Dar es Salaam, aliulizwa kama tayari ameshapokea barua kutoka Marekani ya kumpiga marufuku kuingia nchini humo.

Akijibu sali hilo, Makonda amesema kuwa leo alifika katika kipindi hicho kuzungumzia masuala ya kiserikali si binafsi.

“Hapa nimekuja kama mkuu wa mkoa, subiri nikija binafsi tutajadiliana, nimekuja kama Serikali,” amesema

Tarehe 1, February  2020 Marekani ilieleza kumzuia Makonda kuingia Marekani pamoja na mkewe, Mary na kwamba sababu ni tuhuma za kushiriki kukandamiza haki za binadamu.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527