KAMBI YA KIJESHI YA MAREKANI IRAQ YAPIGWA TENA KOMBORA


Kombora la aina ya Katyusha limeanguka kwenye kituo cha jeshi la Marekani katika mkoa wa Kirkuk, kaskazini mwa Iraq. 

Shambulizi hilo lilitokea Alhamisi jioni bila kusababisha kifo au majeruhi. 

Hata hivyo, kikosi cha polisi cha Iraq kilifanya msako eneo lilikorushwa kombora hilo, na kugundua kifaa cha kurushia makombora chenye makombora kumi na mbili, kombora moja tu likiwa limerushwa.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527