CHELSEA YANASA KIUNGO MWAFRIKa


Hakim Ziyech
Klabu ya Chelsea imekamilisha usajili wa kiungo Hakim Ziyech kutoka klabu ya Ajax ya nchini Uingereza.

Ajax imethibitisha kuwa kiungo huyo raia wa Morocco atajiunga baada ya kumalizika kwa msimu huu, mnamo Julai 1, 2020 baada ya Chelsea kufikia dau la Pauni milioni 45.

Katika ukurasa wa Twitter wa Ajax, umewekwa video inayoonesha maisha ya Ziyech ndani ya viunga vya klabu hiyo yenye mafanikio makubwa nchini Uholanzi, huku ikiambatana na ujumbe, "enyi Chelsea, muamini katika kipaji chake na vitu vikubwa zaidi vitakuja".

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527