KATIBU MWENEZI CHADEMA SHINYANGA MJINI CHARLES SHIGINO AFUKUZWA UANACHAMA CHADEMA

Katibu Mwenezi wa CHADEMA wilaya ya Shinyanga Mjini, Charles Shigino.

CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA)

MKOA WA SHINYANGA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI NA UMMA.

YAH: KUFUKUZWA UANACHAMA NDUGU CHARLES SHIGINO.

Baraza la Uongozi Mkoa Shinyanga, katika kikao chake cha dharula kilichoketi Tarehe 11.02.2020, kimeamua kumfukuza uanachama wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo  (CHADEMA) Ndugu Charles Shigino, aliekuwa Katibu Mwenezi  wa Jimbo la Shinyanga Mjini.

Kwa Mujibu wa Katiba ya CHADEMA ya Mwaka 2006, Toleo la 2016. Ibara ya 5.4. Inaeleza  juu ya “Kukoma kwa Uanachama.” Kwamba, Ibara 5.4. (1 , 2, na 3) inaeleza kuwa; Mwanachama atakoma uanachama wake kwa kujiuzulu , kufariki , kuachishwa ama kufukuzwa.

Kwa mantiki hiyo, Ndugu Charles Shigino, amefukuzwa Uanachama wa CHADEMA, kutokana na kupatikana na makosa ya utovu wa nidhamu na usaliti kwa Chama pamoja na kwenda kinyume cha Katiba ya Chama, Kanuni na Maadili ya Viongozi wa Chama, na hivyo; anakosa sifa ya kuwa Mwanachama wa CHADEMA kwa mujibu wa Ibara ya 5.4.5 ya Katiba ya Chama.

Aidha, Chama kinatoa taarifa kwa Umma na Wanachama kuwa Ndugu Charles Shigino, kuanzia tarehe 11.02.2020, si Mwanachama wa CHADEMA tena.


Imetolewa na;

EMMANUEL NTOBI
MWENYEKITI (M)SHINYANGA
13.02.2020

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527