AFARIKI DUNIA KWA KUPIGWA RADI AKINYOLEWA SALUNI


Martin Nyigu (35) mkazi wa kijiji cha Lusitu, kata ya Luponde, halmashauri ya mji wa Njombe mkoani Njombe,  amefariki dunia kwa kupigwa na radi jana majira ya saa 9 alasiri akiwa ananyoa nywele saluni huku kinyozi na wateja waliokuwa wanasubiri huduma wakiwa salama.

Diwani wa  Luponde, Ulrick Msemwa, amethibitisha ukweli wa taarifa hizo kwa mujibu wa taarifa za awali alizopokea kutoka kwa mtendaji wa kata hiyo, Patrick Mtundu.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527