EBENEZER TV YAMWAGA NAFASI ZA AJIRA...SOMA HAPA UOMBE MARA MOJA


Ebenezer Television ni kituo kipya cha habari ambacho kinatarajia kuanza kurusha matangazo yake kutokea Mikocheni Dar es Salaam. Kituo kinahitaji wafanyakazi katika Nyanja zifauatazo;

A.    NAFASI ZA AJIRA

1.     Mhariri Mkuu – Nafasi moja (1)
-        Awe na Shahada ya Uandishi wa Habari au Mawasiliano ya umma
-        Awe na uzoefu usiopungua miaka mitatu katika nafasi hiyo
-        Awe amelelewa katika maadili ya kikristo.
-        Awe na uwezo wa kusimamia uzalishaji wa vipindi
-        Awe amehitimu katika vyuo vikuu vinavyotambulika na serikali.

2.     Wazalishaji vipindi – Nafasi tatu (3)
-        Awe ana kiwango cha chini cha Stashahada kutoka Chuo kinachotambulika.
-        Awe na uzoefu usiopungua miaka miwili katika nafasi hiyo

3.     Waandishi wa Habari – Nafasi tatu (3)
-        Awe ana kiwango cha chini cha Stashahada kutoka Chuo kinachotambulika.
-        Awe na uzoefu usiopungua miaka miwili katika nafasi hiyo

4.     Wahariri wa picha nyongefu na wasanifu – Nafasi mbili (2)
-        Awe na Stashahada kwenye uandishi wa habari, uhariri picha au ubunifu wa matangazo.
-        Awe na uzoefu usiopungua miaka miwili.

5.     Wapiga picha nyongefu – Nafasi nne (3)
-        Wawe na elimu kuanzia Astashahada katika upigaji picha nyongefu
-        Awe na ujuzi wa sauti za picha nyongefu
-        Awe na uzoefu usiopungua miaka miwili.

6.     Warusha Matangazo – Nafasi tatu (3)
-        Awe na Stashahada katika teknolojia ya Habari na Mawasiliano (ICT)
-        Au Stashahada katika teknolojia ya mawasilianao na elektroniki
-        Awe na uwezo wa kutatua matatizo ya kiufundi
-        Awe na uwezo wa kushauri vifaa bora kutokana na teknolojia

7.     Wasoma Habari – Nafasi tatu (3)
-        Awe na elimu isiyo chini ya Astashahada ya Uandishi wa Habari au sifa inayofanana na hiyo.
-        Awe na uzoefu usiopungua miaka miwili katika fani husika

8.     Mkutubi – Nafasi moja (1)
-        Awe na elimu isiyo chini ya Astashahada ya utunzaji kumbu kumbu
-        Awe ana ujuzi wa kutunza vielelezo vya sauti na picha nyongefu
-        Uzoefu wa zaidi ya mwaka mmoja.

9.     Msimamizi wa vipindi – Nafasi moja (1)
-        Awe na elimu isiyopungua astashahada ya uandaaji na usimamizi wa vipindi
-        Awe anajua kupanga ratiba za vipindi katika kituo cha runinga.
-        Awe anajua kupanga utaratibu wa matukio ya kitaifa au kikanisa yatakayotokea.
-        Awe anajua kupanga na kuratibu matangazo ya biashara katikati ya vipindi pale endapo tangazo litakuja.

10. Mratibu wa maudhui mtandaoni – Nafasi moja (1)
-        Awe na elimu isiyopungua Astashahada
-        Awe na uzoefu wa mitandao ya kijamii
-        Mwenye ujuzi wa mifumo ya kielectronika na komputa

11. Msimamizi wa Utawala – Nafasi moja (1)
-        Awe na elimu ya shahada ya awali katika Uongozi yaani (Public Administration, Leadership and Governance.
-        Mwenye ujuzi wa habari na Mawasiliano atapewa kipaumbele
-        Awe amelelewa katika maadili ya dini ya KIKRISTO
-        Awe tayari kufanya kazi nyingine zinazoendana na nafasi hyo
-        Awe na uwezo wa kufanya tathmini ya wafanyakazi waliopo na kushauri Uongozi njia bora ya kuboresha.
-        Uzoefu wa miaka miwili katika nafasi kama hyo

12. Mhasibu – Nafasi moja (1)
-        Awe na elimu ya shahada ya awali katika masuala ya fedha
-        Awe amelelewa katika maadili ya kikristo
-        Awe na uelewa katika masoko na biashara
-        Awe na uzoefu wa miaka miwili
-        Awe amelelewa katika maadili ya KIKRISTO

13. Fundi sanifu wa umeme – Nafasi moja (1)
-        Awe na stashahada ya umeme katika chuo kinachotambulika
-        Awe na uzoefu wa vifaa vya electronics na sauti
-        Awe anaufahamu umeme wa phase moja na phase tatu
-        Awe na uwezo wa kufuatilia tatizo la umeme na kulitatua
-        Awe na ujuzi wa kuunganisha na kuwasha generator.



B.    NAFASI  ZA WAKURUFUNZI (INTERNS)
1.     Waandishi wa Habari – Nafasi tatu (3)
2.     Mhariri wa picha – Nafasi mbili (2)
3.     Msaidizi wa msimamizi wa vipindi – Nafasi mbili (1)
4.     Mrusha Matangazo – Nafasi mbili (2)
5.     Wapiga picha – Nafasi mbili (2)
6.     Wakutubi – Nafasi mbili (1)
7.     Waandaaji vipindi – Nafasi mbili (2)

-        Wawe na ujuzi katika fani husika uzoefu si lazima AU awe mwanafunzi anayetarajia kumaliza masomo katika fani husika

C.    Watendaji wa kujitolea (Volunteers)
1.     Wapiga picha – Nafasi 1
2.     Wahariri picha – Nafasi 3
3.     Waandaaji vipindi – Nafasi 4
4.     Afisa Masoko – Nafasi 3


Maombi yote yaliyo ambatanishwa na nakala za vyeti na CV yatumwe kwa;
Mratibu wa Mradi - Ebenezer Television
S.L.P 4067
Shule Kuu ya Uandishi wa Habari na Mawasiliano ya Umma
Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam.
Dar es Salaam.

AU


Kwa barua pepe ebztvtz@gmail.com katika mfumo wa PDF na viambatanisho vyote viwe katika nakala moja. Mwisho wa kutuma maombi ni February 12, 2020.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527