DKT. ABBAS KUENDELEA KUWA MSEMAJI WA SERIKALI


Rais  Magufuli ametaja sababu ya kumteua Dk Hassan Abbasi kuwa katibu mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo akisema ni kutokana na kufanya kazi nzuri ya kuisemea Serikali bila kuchoka. Kabla ya uteuzi huo, Dk Abbasi alikuwa msemaji mkuu wa Serikali.

“Dk Abbas amefanya kazi nzuri kama msemaji wa Serikali, hakuchoka aliisemea vizuri Serikali, ningependa aendelee tu kuwa msemaji wa Serikali lakini mahali mtu anapotakiwa kupata promosheni, usimnyime promosheni.

“Ndiyo maana tumemteua awe katibu mkuu wa wizara hiyo na kwa sasa hivi ataendelea kuwa msemaji wa Serikali mpaka tutakapopata mwingine na atakuwa anasema sasa akiwa mkubwa zaidi,” amesema Magufuli.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post