TRUMP ATISHIA KUIWEKEA IRAQ VIKWAZO KAMA ITAWAFUKUZA WANAJESHI WA MAREKANI

Rais wa Marekani, Donald Trump, ametishia kuiwekea Iraq vikwazo baada ya bunge la nchi hiyo kupiga kura kupitisha azimio linalovitaka vikosi vya Marekani viondoke nchini humo. 

Trump amesema iwapo wanajeshi hao wataondoka, Iraq itapaswa kuilipa Marekani gharama za kambi ya jeshi la anga iliyoko Iraq. 

Trump amebainisha kuwa hawatoondoka hadi hapo Iraq itakapoilipa Marekani gharama za kambi hiyo ambayo amesema iko muda mrefu hata kabla ya wakati wake na iligharimu mabilioni ya dola kuijenga.

 Trump amesema kama Iraq itavitaka vikosi vya Marekani kuondoka na suala hilo kufanyika katika njia isiyokuwa na misingi ya kirafiki, basi nchi yake itaweka vikwazo vikali kwa Iraq ambavyo haijawahi kushuhudia.

 Wakati huo huo, Ikulu ya Marekani imesema kuwa Trump amezungumza na Waziri Mkuu wa Uingereza, Boris Johnson kuhusu hali inayoendelea nchini Iraq na Iran.

Soma hii: Ajira Mpya 250+ zilizotangazwa wiki hii

Mvutano bado ni mkubwa baada ya Marekani kuusika kumuua kiongozi wa jeshi wa Marekani jenerali Qasem Soleimani huko Baghdad wiki iliyopita.

Soleimani ambaye alifariki akiwa na umri wa miaka 62, alikuwa akiongoza operesheni za vita katika nchi za mashariki ya kati

Kiongozi mpya wa kikosi cha jeshi la Iran la Quds - ambacho Soleimani aliongoza - ameapa kuwaondoa Wamarekani katika mataifa ya mashariki ya kati.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527