NYOTA WA ZAMANI WA LA LAKERS KOBE BRYANT AMEFARIKI DUNIA KATIKA AJALI


Nyota wa mpira wa vipaku nchini Marekani Kobe Bryant amefariki dunia pamoja na wenzake wanne kwenye ajali ya helikopta iliyotokea California usiku wa leo tarehe 26 Januari 2020.

Taarifa kutoka Marekani zimeeleza kuwa Kobe Bryant alikuwa akisafiri kwa helikopta binafsi kabla haijalipuka na kuteketea kwa moto huko Calabasas.

Kwa mujibu wa Mamlaka jijini Los Angeles wameeleza kuwa jumla ya watu watano walikuwa kwenye helikopta hiyo na hakuna aliyenusurika katika ajali hiyo.

Kobe Bryant amefariki akiwa na umri wa miaka 41 akiwa na ameichezea timu ya mpira wa kikapu ya Los Angeles Lakers nchini Marekani kwa takribani miaka 20, hadi alipostaafu mwezi Aprili mwaka 2016


Rais wa zamani wa Marekani Barack Obama ni  miongoni mwa watu wa awali mashuhuri waliotuma salamu za rambirambi kufuatia kifo  hicho.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527