MUME ATOLEWA UTUMBO NJE NA MKEWE KISA KUHOJI MATUMIZI YA SHILINGI ELFU 10 ALIYOACHA


Benedictor Gogogo (48) mkazi wa Itabagumba, Sengerema mkoani MWANZA amechanwa tumbo na kitu chenye ncha kali hadi utumbo kutoka nje baada ya kutokea ugomvi kati yake na mke wake


Kamanda wa Polisi Mkoani humo, Jumanne Murilo amesema tukio hilo lilitokea jana na wanamashikilia Mtuhumiwa kwa mahojiano na uchunguzi zaidi

Akiwa hospitalini, Gogogo amesema mzozo kati yake na mke wake aliyemtaja kwa jina la Mama Asteria ulitokana na kuhoji matumizi ya Tsh. 10,000 aliyoacha nyumbani asubuhi ya siku hiyo

Amesema, “Wakati naondoka kwenda kwenye shughuli zangu za uvuvi, asubuhi ya siku ya tukio, niliacha Tsh. 10,000 ya matumizi. Niliporejea nilimwomba anipe Tsh. 1,000 ninunulie vocha ya simu lakini akaniambia fedha yote imeshatumika.”

Ameongeza, “Nilipohoji zaidi akaanza kunitolea majibu yaliyonikasirisha na kunifanya nimpige kofi na kutokea mzozo kati yetu ambao hata hivyo uliisha na mimi kuingia ndani kujipumzisha.”

Aidha, Gogogo ameeleza kuwa akiwa ameanza kupitiwa usingizi, mke wake ambaye wameishi mwaka mmoja na nusu sasa alimvizia na kumchana na kitu chenye ncha kali tumboni hadi utumbo kutoka nje


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post