JAMAA ANYWA MIKOJO YA WANAWAKE LITA MOJA NA NUSU


Jamaa mmoja nchini Uganda aliyetambulika kwa jina la Ismail Dholaga mwenye miaka 35, amelazimika kunywa lita moja na nusu ya mikojo ya wanawake ili kurejesha fahamu baada ya kulewa tilalila.

Ismail Dholaga ambaye anafanya kazi ya udereva wa pikipiki (bodaboda) alilazimishwa kufanyiwa kitendo hicho na wakazi wa eneo la mji wa Iganga, baada ya kukutwa akiwa amelewa na wapita njia.

Wakazi wa eneo hilo na wapita njia walikusanya mikojo ya wanawake waliokuwepo kwenye tukio, ikapatikana lita moja na nusu, mmoja wa wanawake waliotoa huduma hiyo amesema “Tulifaulu kupata lita moja unusu ya mkojo na kumlazimisha kunywa kama huduma ya kwanza”.

Hata hivyo huduma hiyo haikufanikiwa ndipo maafisa wa polisi walifika na kumkimbiza katika hosptali iliyokuwa karibu.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527