TCRA : TUNAZIMA KIDOGO KWA SABABU YA MAMBO YA KITAALAMU, HAUWEZI UKAZIMA LAINI MILIONI TANO AU 10 KWA MARA MOJA


Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), James Kilaba amesema uzimaji wa laini za simu ambazo hazijasajiliwa kwa alama za vidole unafanyika kwa Awamu.

Amesema zoezi hilo lililoanza jana Januari 20, 2020 linafanyika kwa Awamu ili kuondoa usumbufu na hadi kufikia jana usiku saa nne walikuwa wamezima laini 975,041

Amesema, kundi la kwanza waliozimiwa laini ni watu 656,091 ambao wana Vitambulisho vya Taifa au Namba lakini hawajasajili laini zao

Amebaisha kuwa, kundi la pili ni watu 318,950 waliosajili laini zao kwa Kitambulisho cha Taifa kabla ya kuanza mfumo wa kusajili kwa Alama za Vidole

Amesema, “Tunazima kidogo kwa sababu ya mambo ya kitaalamu, hauwezi ukazima laini milioni tano au 10 kwa mara moja kwa maana watajazana kwenye kusajili kitu kinachofanya Mifumo ya NIDA inaelemewa"


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527