IRAN YAWAKAMATA WALIOIDUNGUA KIMAKOSA NDEGE YA UKRAINE


Msemaji wa idara ya sheria ya Iran Gholamhossein Esmaili amesema, Iran imekamata baadhi ya watu kutokana na kuhusika kwao katika ajali ya ndege ya Ukraine iliyosababisha vifo vya watu 176 waliokuwa ndani ya ndege hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari, Bw. Esmaili amesema mpaka sasa uchunguzi kuhusu wahusika umefanyika, na wataalamu wa sheria wanajitahidi kuhoji, kuchunguza na kukusanya taarifa.

Amesema sanduku jeusi limepelekwa Ufaransa, na wataalamu wa Iran na Ukraine watashiriki kwenye kazi ya kusoma data.

Jumamosi wiki iliyopita, jeshi la Iran lilisema, limeangusha kwa makosa ndege ya abiria ya Ukraine, na kosa hilo la kibinadamu linapaswa kulaumiwa.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527