IRAN YAAPA KULIPIZA KISASI KWA MAREKANI KUFUATIA MAUAJI YA KAMANDA MKUU WA JESHI LAKE LA QUDS


Kiongozi mkuu wa Iran Ayatollah Ali Khamenei amesema, nchi hiyo itajibu vikali mauaji ya kamanda wa Kikosi cha Mapinduzi ya Kiislam (IRGC) Meja Jenerali Qassem Soleimani.

Khamenei amesema lengo la Soleimani na harakazi zake za ukombozi hatitasimama kutokana na kifo chake, bali zitaendelea kwa nguvu zaidi, na ushindi dhahiri unawasubiri wale wanaopigana katika njia hiyo.

IRGC leo imethibitisha kuwa, Meja Jenerali Soleimani ameuawa katika shambulizi la anga lililotokea katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Baghdad.

Kiongozi huyo ametangaza siku tatu za maombolezo kufuatia kifo cha Soleimani.

Wakati huohuo, Wizara ya Ulinzi ya Marekani imesema, jeshi lake lilifanya shambulizi lililomuua kamanda huyo wa IRGC.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527