KUKU ALIYEUA MTOTO AUAWA KWA KUSHAMBULIWA NA WANANCHI


Wazazi wa mtoto aliyeuawa kwa kushambuliwa na kuku

Moja ya taarifa kutoka maeneo ya Malava Kaunti ya Kakamega nchini Kenya zinasema Kuku aliyemuua mtoto wa miezi 6 ameshambuliwa hadi kufa na wanakijiji wa eneo hilo.

Inadaiwa kuwa mtoto huyo alifariki nyumbani kwao kwa mshtuko baada ya kushambuliwa na kuku ambaye alikuwa anajaribu kuwalinda vifaranga vyake.

Kulingana na ripoti iliyotolewa na tovuti ya The Standard, Mama wa mtoto huyo aitwaye Robai Toboko amesema, familia imebaki na majonzi kwa mtoto wake huyo wa miezi 6 kufariki akiwa mikononi mwake .

"Nilikuwa nimempakata mwanangu, katika ile harakati yake kujaribu kumkamata mmoja wa vifaranga, kuku huyo alimrukia mtoto kwa hasira na kumgonga usoni na bawa lake. Mtoto alishtuka na akaanza kulia kwa muda mrefu kisha akapoteza fahamu" ameeleza mama wa mtoto

Aidha amesema mtoto wake alikuwa yupo vizuri kiafya ila alikata roho baada ya kupata mshtuko wa kushambuliwa na kuku, pia majirani walijitokeza kumsaidia japokuwa walikuwa wamechachelewa lakini walimuua kuku huyo pamoja na vifaranga vyake.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527