NAIBU WAZIRI MASAUNI AAGIZA MKUU WA CHUO CHA POLISI DAR AONDOLEWE NA ASHUSHWE CHEO


Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Hamad Masauni amemtaka Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) Simon Sirro kufanya mabadiliko ya uongozi kwenye Chuo cha Polisi Dar es Salaam kutokana na kukiuka maagizo yake katika ujenzi wa mabweni chuoni hapo.

Pia, Masauni amemuelekeza IGP Sirro kumuondoa Mkuu wa Chuo hicho, Antony  Ruttashuburugukwa na kumshusha cheo kutokana na kosa hilo.

Akizungumza leo Jumatano Novemba 27, 2019 akiwa chuoni hapo, Masauni amesema alielekeza katika ujenzi huo watumike wafungwa kufanya kazi za vibarua ili kuokoa fedha lakini mkuu huyo wa chuo hakutekeleza agizo hilo.

“Rais alikubali kutupatia Sh700 milioni kwa ajili ya ujenzi wa mabweni, tuliangalia na kuona tunaweza kuokoa Sh210 milioni za kuwalipa vibarua kwa kuwatumia wafungwa.”

“Nilizungumza na kamishna wa magereza akasema hilo linawezekana hivyo nikamuelekeza mkuu wa chuo kufanyia kazi suala hilo lakini leo nimekuja nakuta hali hii hakuna wafungwa,” amesema Masauni

Wakati Masauni anakagua ujenzi huo alikuta vijana wakifanya kazi na alipowahoji walimuleza kuwa wao ni vibarua wanaolipwa kwa siku.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527