POLISI YACHUNGUZA KIFO CHA MWANAFUNZI WA DARASA LA SITA KUTOA MIMBA


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Simon Maigwa, amesema kuwa bado wanachunguza chanzo kufuatia kifo cha Mwanafunzi wa darasa la sita katika Shule ya Msingi Mtumbatimaji, anayedaiwa kufariki baada ya kutoa mimba.

Akizungumza na EATV&EA Radio Digital leo Novemba 8, 2019, Kamanda Maigwa amesema kuwa binti huyo alifikishwa hospitalini akiwa tayari anavuja damu, hivyo bado wanafanyia uchunguzi kwa sababu hata mama mzazi wa binti huyo bado hajatoa maelezo ya kina.

"Ni kweli hili tukio limetokea na bado tunachunguza lakini alipelekwa hosptali na wazazi wake akiwa tayari anavuja damu na baada ya kukaa hospitali akiendelea na matibabu akafariki, mama yake wakati anajaribu kuhojiwa alikuwa anazimia sasa ni masuala ya kibindadamu inabidi kumuacha mtu atulie", amesema Kamanda Maigwa.

Aidha Kamanda Maigwa ameongeza kuwa mara baada ya uchunguzi wa tukio hilo kukamilika, Jeshi la Polisi litatoa taarifa ya kina kuhusu kifo hicho.
Chanzo - EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527