TUNDU LISSU AMEPONA LAKINI ANAHOFIA USALAMA WAKE KURUDI TANZANIA


Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, imeelezwa kuwa aliyekuwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu ameshapona ila anashindwa kurudi nchini kwa kile alichokidai ni kuhofia usalama wake.

Hayo yameelezwa leo Novemba 21,2019 na Mdhamini wa Lissu, Ibrahim Ahmed, alipokuwa akiieleza mahakama hiyo juu ya afya ya Mwanasheria huyo wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Ahmed ameieleza mahakama hiyo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, wakati wa kesi ya uchochezi inayomkabili mshtakiwa huyo na wenzake watatu ilipoitwa.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527