KIJANA ALIYEMTISHIA MWENZAKE KWA BASTOLA AFIKISHWA MAHAKAMANI


Kijana Shaban Hamisi amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni akikabiliwa na kosa la kumtishia silaha  Dereva wa lori la mchanga Venance John ikiwa ni siku chache baada ya kusambaa mitandaoni video ya tukio.

Amesomewa mashtaka yake na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Mkunde Mshanga mbele ya Hakimu Mfawidhi, Frenk Moshi, ambapo inadaiwa tukio hilo amelitenda Oktoba 30, 2019 maeneo ya Mbezi Mabwepande.

Inadaiwa alikutwa na Pistol aina ya Berreta yenye namba za usajili 102969 ambapo kwa makusudi alimtishia Venance John huku akijua kufanya hivyo ni kosa kisheria, baada ya kusomewa shtaka alikana ambapo pia upande wa mashitaka umesema hauna pingamizi na dhamana.

Baada ya kueleza hayo, Hamisi ambae pia ni Mume wa Mtangazaji Zamaradi Mketema ameachiwa kwa dhamana ya Wadhamini wawili wenye barua na vitambulisho vya Taifa na wamesaini Bondi ya Sh.Mil 2 kwa kila mmoja, kesi imeahirishwa hadi November 13, 2019, mshitakiwa yupo nje kwa dhamana.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527