CHADEMA WAITAKA SERIKALI KUTOTUMIA JINA NA NEMBO YA CHAMA CHAO KWENYE UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA


Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetaka Serikali kutotumia nembo na jina la chama hicho kwenye karatasi za kupigia kura katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba 24, mwaka huu.

Naibu Katibu Mkuu (Bara), wa chama hicho, John Mnyika amesema amesema hayo leo Jumapili Novemba 10, jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Amesema sababu ya uamuzi huo ni kutokana na wao kujiengua katika kinyang’anyiro hicho hivyo wagombea wao wasiwepo katika fomu hizo za kupigia kura.

“Kesho Novemba 11, tutamuandikia barua Waziri wa Tamisemi (Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa), Suleiman Jaffo, kuacha kutumia jina nembo ya chama chetu.

“Pia tunamuomba Rais Dk. John Magufuli, kuingilia kati ukiukwaji wa sheria unaoendelea kwenye uchaguzi huo kama alivyohamasisha wakati wa uandikishaji,” amesema Mnyika.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527