ALIYEMTISHIA MWENZAKE KUMUUA KWA BASTOLA AKAMATWA


Kamanda wa Polisi Kinondoni, Mussa Taibu amesema wamemkamata Shabani Hamis Said ambaye anadaiwa kumtishia kwa Bastola dereva wa lori Venance John maeneo ya Mabwe Pande, saa 3 asubuhi, October 30, 2019.

Amesema baada ya lori la mchanga  alilokuwa anaendesha Venance kukwama bila kupata msaada wa haraka, akatokea mshtakiwa Shabani Hamis akiwa anaendesha gari lake aina ya Subaru na kumtaka dereva huyo ampishe ili apite na  akamjibu hawezi kumpisha kwa sababu amekwama katika mchanga.

Baadae wananchi wakatokea na kumpa msaada wa kumkwamua na kuondoka lakini alipofika mbele mshtakiwa alimzuia dereva huyo wa lori na kuanza kumtupia maneno kisha wakaanza kujibizana na kufikia hatua ya mshitakiwa kuamua kutoa Bastola na kutishia kumuua Venance.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527