SERIKALI YASAINI MKATABA WA UNUNUZI WA NDEGE MPYA YA BOMBARDIER Q400


Serikali ya Tanzania imesaini mkataba na kampuni ya kutengeneza ndege kutoka Canada kwa ajili ya ununuzi wa ndege mpya aina ya Bombardier Q400, inayotarajiwa kufika nchini June 2020, yenye uwezo wa kubeba abiria 78.



Mkataba huo umesainiwa leo Jumamosi Oktoba 19, 2019 lengo likiwa ni kuimarisha na kuboresha utoaji huduma za usafiri wa anga nchini kupitia Shirika la Ndege Tanzania (ATCL).

Mtendaji mkuu wa Wakala wa Ndege za Serikali, Dk Benjamin Ndimila amesema ndege hiyo itakua na uwezo wa kutua hata kwenye viwanja vya vumbi.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527