RAIS MAGUFULI AMTUMBUA MKUU WA WILAYA NA MKURUGENZI WA HALMASHAURI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Mkuu wa Wilaya ya Nachingwe Rukia Muwango, pamoja na Mkurugenzi wa Wilaya hiyo Bakari Mohamed Bakari, ambaye nafasi yake imechukuliwa na Hassan Abbas Rungwa.

Taarifa hiyo imetolewa Oktoba 19, 2019, na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Gerson Msigwa, ambapo nafasi ya Mkuu wa Wilaya imechukuliwa na Hashim Abdallah Komba.

Uteuzi mwingine ambao umefanywa na Rais Magufuli leo ni wa Godfrey Mweli, ambaye amekuwa Naibu katibu mkuu TAMISEMI, akichukua nafasi ya Mathias Kabunduguru ambaye amekuwa Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania.

Katika hatua nyingine Rais Magufuli amemteua Mathias Kabunduguru, kuwa mtendaji mkuu wa Mahakama ya Tanzania, akichukua nafasi ya Hussein Katanga ambaye ameteuliwa kuwa Balozi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527