Breaking : MCHUNGAJI WA KANISA LA VICTORIA ASHAMBULIWA NA WATU WASIOJULIKANA...YUPO HOI




Mchungaji Amos Joseph kutoka kanisa la Victoria Itobo wilaya ya Nzega mkoani Tabora amenusurika kufa baada ya kushambuliwa na kundi la vijana wasiojulikana leo alfajiri Jumamosi Septemba 7,2019 katika Manispaa ya Tabora.

Kwa Mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo wameiambia Malunde 1 blog kuwa Mchungaji huyo amekutwa akiwa hoi amelala hawezi kusimama pembezoni mwa shule ya msingi Mabatini Manispaa ya Tabora mkabala na barabara kuu kutoka Kigoma kwenda Dar es salaam.

"Tumezungumza nae japo haongei sana anasema amefika Mjini Tabora akitokea Itobo wilaya ya Nzega, alikuja Tabora kumtafuta mke wake aliyetoroka nyumbani na kumwachia mtoto. Alipofika Tabora leo amekumbana na vijana wakitaka pesa,wakamshambulia kisha kuchukua pesa na simu zake",ameeleza mmoja wa mashuhuda hao. 

Tayari wasamaria wema wamejitokeza kumsaidia na taratibu za kumpatia matibabu zinaendelea.
Huyu ni mchungaji Amos Joseph kutoka kanisa la Victoria Itobo,amepatikana alfajiri barabara kigoma - Dar hapa jirani na shule ya msingi Mabatini manispaa ya Tabora,ameshambuliwa kwa kupigwa sana kiasi hawezi hata kusimama,kimsingi yupo hoi.Msaada wa haraka unahitajika bado yupo hapa pembeni ya barabara amelala

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527