MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AMWAKILISHA RAIS MAGUFULI KUAGA MWILI WA MAREHEMU KADUMA.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo Sept 03,2019 amemuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe magufuli kwenye Shuhuli ya kuaga Mwili wa Mwanasiasa Mkongwe Nchini Marehemu Ibrahim kaduma.



Katika salam zake za pole kwa Wanafamilia, wafiwa na Watanzania wote kwa Ujumla, Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan amewaomba kuwa na Subira na Uvumilivu katika kipindi hiki cha Maombolezo na kumuomba Mwenyezi Mungu kuwapa nguvu na Moyo wa Subira.

Wakati wa Uhai wake Marehemu Ibrahim Kaduma aliwahi kuwa Mwanasiasa pamoja na kupitia ngazi mbali mbali za Uongozi hapa nchini.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527