LUGOLA AAMURU NABII ELIYA MAHELA AKAMATWE

Waziri wa Mambo ya Ndani Kangi Lugola ametua katika kanisa Pentecostal Power Ministry na kuamuru kukamatwa kwa Mchungaji wa kanisa Hilo Nabii Eliya Mahela kwa kosa la kuendesha kanisa bila kusajili

wa na kupiga kelele kwa Wananchi wanaomzunguka. 




Uamuzi wa kukamatwa kwa Nabii Mahela umetolewa leo Jumatatu Septemba  9, 2019  na Waziri Lugola baada ya kufanya ziara katika kanisa hilo kufuatia malalamiko ya mara kwa mara kutoka kwa majirani dhidi ya kanisa hilo.


Amesema majirani wa eneo hilo kwa nyakati tofauti wamekuwa wakilalamika kelele zinazotoka kanisa hilo na licha ya viongozi wa Serikali kumpa onyo la kujirekebisha mchungaji huyo hakufanya hivyo.

"Ulikuwa ukiwaambia wananchi kuwa ujali na waende kokote leo kokote zimefika 40. Kokote nipo hapa na kokote hutopona," amesema Lugola.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527