FAIZA ALLY AFUNGUKA BAADA YA SUGU KUOA MWANAMKE MWINGINE


Mzazi mwenza wa Mbunge wa Mbeya Mjini Sugu, Faiza Ally amesema amependezwa na tukio la kufunga ndoa kwa Joseph Mbilinyi, na anaamini sasa Mbunge huyo anaenda kuwa na maisha ya furaha zaidi.

Faiza ametoa kauli hiyo ikiwa saa chache baada ya Mbunge Sugu kufunga ndoa na mkewe Happines Msonga, ambapo kupitia mtandao wake wa Instagram, amesema licha ya Sugu kuoa bado ana mapenzi na yeye.

"Kuna mtu anayenipemnda sana alinipa ratiba nzima mwezi mmoja kabla ya ndoa na kabla ya hapo nilijua kama wataoana ila siku ya tukio ni siku ya tofauti, hata mwanzoni nilipotaka kufanya jambo nilijikuta nakosa hisia za kufanya kwa sababu sina tena majonzi juu ya baba Sasha.", amesema Faiza.

Ameendelea kusema, "nikimwangalia baba Sasha na mke wake sioni mtu wa kuniliza na najiuliza nilikosea wapi, kwa sababu nilikuwa mpenzi bora, nilikuwa mama bora kwahiyo sijapata mwanaume tu wa kunielewa mimi. Anaoa lakini najua bado ananipenda mimi".

Mapema jana Agosti 31, 2019 Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi 'Mr.II Sugu' alifunga ndoa na mpenzi wake Happiness Msonga, katika kanisa Katoliki, Ruanda jijini Mbeya.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527