ALIYENASWA AKIFANYA MAPENZI NA MWANAFUNZI NDANI YA CHUMBA CHA MAMA YAKE ATUPWA JELA MIAKA 30


Mkazi wa Kata ya Mikumbi, Halmashauri ya Manispaa ya Lindi, Abdull Mohamedi (30) amehukumiwa kifungo cha miaka (30) Gerezani, baada ya kupatikana na hatia ya kukutwa na hatia ya kujihusisha kimapenzi na mwanafunzi wa Shule ya Sekondari.

Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu wa Mahakama ya Mkoa huo, James Karymaha baada ya kuthibitisha bila shaka na ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka.

Hakimu Karyamaha akitoa hukumu katika kesi hiyo namba 08/2019 kupitia kifungu cha Sheria namba 130 kifungu kidogo (1) na (2) na 131 kifungu cha (2) amesema kutokana na kubanwa na Sheria amemuhukumu kifungo cha miaka 30 gerezani.

Awali ilidaiwa mahakamani hapo na Mwanasheria wa Serikali Abdulaha Madi Mohamedi kuwa mshitakiwa alikamatwa na mama mzazi wa mwanafunzi huyo Salma Salum, Julai 05, 2019, akiwa chumbani ndani ya nyumba yake na mtoto wake akishiriki mapenzi.

Mwanasheria huyo wa Serikali, amesema baada ya Mama mzazi kumkuta mshtakiwa akiwa na mtoto wake alitoa taarifa kwa uongozi wa Serikali ya Mtaa na Kata yao na majirani, ambao walifika na kufanikiwa kumkamata na kumfikisha kituo cha Polisi.

Kabla ya Jaji Ngwembe hajatoa adhabu hiyo, mshtakiwa alipewa nafasi ya kujitetea na kuomba imuonee huruma kwa kutompa adhabu kali, kwa madai ni mkosaji wa mara ya kwanza na pia shetani mbaya wa mapenzi alimpitia.
Chanzo - EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527