WAZIRI WA KILIMO JAPHET HASUNGA AONGEZA SIKU TATU MAONYESHO YA NANE NANE SIMIYU


Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga, ameongeza siku tatu kuendelea kuwepo kwa maonyesho ya sikuu ya wakulima kitaifa (Nanenane), kuanzia kesho Ijumaa Agosti 9, hadi jumapili ya wiki hii.


Waziri Hasunga ametangaza uamuzi huo wakati akiongea kwenye kilele cha maonyesho hayo mbele ya Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa, ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo iliyofanyika kwenye viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu.

Hasunga amesema kuwa uamuzi huo unatokana na wakuu wa mikoa ya Mara, Shinyanga na Simiyu ambao ndiyo waandaji wa maonyesho hayo kanda ya Magharibi kutaka kuongezewa muda.

“Nilipokea ombi la wakuu wa mikoa ya Mara, Simiyu na Shinyanga ambao ndiyo waaandaaji wa maonyesho haya, wakitaka kuongezewa siku, nami kwa mamlaka niliyopewa nimekubali ombi lao na kuongeza siku tatu hadi jumapili ya wiki hii ndiyo yamalizike,” amesema Hasunga.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527