WAZIRI SIMBACHAWENE AIELEZEA YA KAMATI BUNGE MCHAKATO WA TATHMINI YA ATHARI KWA MAZINGIRA


Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) leo Agosti 27, 2019 imewasilisha taarifa zake mbili kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira jijini Dodoma.

Taarifa zilizowasilishwa ni ya Utekelezaji wa Maazimio ya Bunge yanayohusiana na majukumu ya Wizara yaliyotokana na Mapendekezo ya Kamati hiyo katika taarifa yake ya mwaka iliyowasilishwa katika Mkutano wa Bunge wa Februari 2019.

Kamati hiyo inayoongozwa na Mwenyekiti wake Mhe. Suleiman Sadik pia imepokea taarifa ya Mazingira kwa ajili ya kujijengea uelewa kuhusu Tathmini ya Athari ya Mazingira (TMA). 


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527