WATUMISHI WA UMMA NA SEKTA BINAFSI WAKUMBUSHWA SWALA LA MAADILI

Na Amiri kilagalila-Njombe
Serikali imewataka watumishi wa umma na sekta ninafsi kuzingatia kanuni na maadili ya utumishi wa Umma kwa lengo la kuleta ustawi kwa jamii katika utoaji wa huduma bora na stahiki kwa wahitaji.


Agizo hilo linakuja wakati kukiwa na malalamiko kadha wa kadha kutoka kwa baadhi ya wananchi juu ya utendaji na uwajibikaji mbovu kwa baadhi ya watumishi wa umma ambapo imedaiwa kuwepo kwa anguko la maadili ya utumishi wa umma hatua ambayo imeleta athari kwa umma na kuhitaji hatua za haraka kuchukuliwa kuanzia vyuoni.

Akizungumza katika mahafali ya 4 ya chuo cha afya cha Mgao mkoani Njombe kaimu mganga mkuu wa mkoni Njombe Dr Manyanza Mponeja amewataka wahitimu wa kozi mbalimbali za afya chuo hapo kuzingatia miiko na mdaadili ya kazi pindi watakapo kuwa kazi kwa madai ya kwamba katika miaka ya hivi karibuni kumekuwa na madai ya kuporomoka kwa maadili ya utumishi wa umma hususani katika kada ya afya watu kutumia lugha chafu kwa wagonjwa ,mavazi yasiyo na staha pamoja na ulevi kupindukia hatua ambayo si njema.

Mbali na changamoto ya maadili Dr Mponeja ametolea ufafanuzi ombi la kuondolewa kwa gharama ya shilingi elfu 50 wanayotakiwa kulipa wanafunzi katika hospitali,vituo vya afya na zahanati ambazo wanaenda kujifunza elimu kwa vitendo ambapo amesema serikali imeipokea changamoto hiyo na kwenda kuangalia namna ya kuiondoa ili kutoa nafasi kwa wanafunzi hata wenye hali duni kupata mafunzo hayo muhimu.

“Sitegemei muuguzi ambaye anaandaliwa kukutana na mteja anayemweleza siri zake zote aweze kumtatulia akawa anavaa nguo fupi kiasi ambacho hata mteja anaanza kujiuliza”alisema Mponeja

Licha ya serikali kuahidi kutafuta ufumbuzi wa gharama elimu kwa vitendo inayotolewa na wanafunzi wa vyuo binafsi vya afya lakini afisa utumishi wa chuo cha afya cha mgao Deus Kuba anafafanua jinsi tozo hiyo inavyokwamisha jitihada za wanafunzi wanaotoka familia duni huku pia akionyesha kuwa tofauti na mitazamo ya ukosefu wa ajira katika sekta ya afya kwa kuwa watu wazaliwa na kuumwa kila uchwao hivyo wahitimu wanauwezo wa kufungua maduka ya dawa na phamasi binafsi na mkono kwenda kinywani.

“Wanafunzi wetu wanavyoenda kufanya mazoezi ya vitendo mahospital hususani ya serikali,utakuta kila mwanafunzi huwa anatakiwa kuchangia  gharama ya shilingi elfu 50,unakuta wengine wanashindwa hivyo ningependekeza hizi gharama aidha zitolewa au zipunguzwe”alisema Deus Kuba

Kwa upande wao wahitimu wa kozi mbalimbali za afya akiwemo  Evancy Machea na Hapness Amon wakieleza jinsi walivyo iva kwa ajili ya kutoa huduma kwa jamii na kumudu ushindani katika soko la ajira wamesema wamejengewa uwezo hata wakujiajiri kwa kufungua maduka ya dawa na phamasi.

Jumla ya wahitimu 59 wamehitimu na kukabidhiwa vyeti katika mahafali ya nne ya chuo cha afya Mgao.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527