WATUHUMIWA WATANO WAENDELEA KUSAKWA KWA TUHUMA ZA KUMTEKA MO DEWJI


Upande wa mashtaka katika kesi ya kutekwa kwa mfanyabiashara Mohamed Dewji ‘Mo’ umedai kuendelea na taratibu za kuwatafuta watuhumiwa watano ili kuwaunganishwa katika kesi hiyo.

Hayo yameelezwa leo Jumanne Agosti 20, 2019 na wakili wa Serikali mwandamizi, Wankyo Simon katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Amesema upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika na wanaendelea kuwatafuta watuhumiwa hao watano raia wa Msumbiji na Afrika Kusini.

Watuhumiwa hao ni Henrique Simbue, Daniel Berdardo Manchice,Issac Tomu na Zacarious Junior wote raia wa Msumbiji na Phila Tshabalala raia wa Afrika Kusini.

Baada ya maelezo hayo Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi aliahirisha shauri hilo hadi Septemba 3, 2019.

Mshitakiwa wa kwanza katika kesi hiyo ni Dereva taksi, Mousa Twaleb (46).


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527