WALIOFARIKI AJALI YA MOTO MOROGORO WAFIKIA 75


Majeruhi wanne kati ya 43 wa ajali ya Lori lililolipuka Morogoro waliohamishiwa hospitali ya Taifa ya Muhimbili wamefariki  na kufanya idadi ya waliofariki kufika 75 huku 39 waliobaki wakiendelea kupatiwa matibabu.

Taarifa hii imetolewa na mkuu wa kitengo cha Habari na mawasiliano Muhimbili Bw.Aminiel Aligaesha.


Kuhusu hali za majeruhi mkuu huyo wa kitengo cha mawasiliano amesema wanaendelea vizuri na wapo wanaoonyesha matumaini.

“Tumepoteza wenzetu wengine wanne na miili yao imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti hivyo kama kuna ndugu wa karibu waje kwa ajili ya kuwatambua ndugu zao,” amesema Aligaesha.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527