Vifo ajali ya lori la mafuta Morogoro vyafika 101

Idadi ya vifo vya majeruhi wa ajali ya lori la mafuta iliyotokea mkoani Morogoro, imefika 101 baada ya majeruhi mmoja aliyekuwa akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) kufariki dunia usiku wa kuamkia jana.

Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano MNH, Aminiel Aligaesha, alisema aliyefariki dunia ni Sadiki ismail (31).

Alisema mpaka sasa kati ya majeruhi 47 waliofikishwa hospitalini hapo, waliobaki ni 14 ambapo kati yao 11 wako katika Vyumba vya Uangalizi Maalum (ICU) na watatu wako katika wodi za kawaida na hali zao zinaendelea vizuri.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post