TETESI ZA SOKA LEO JUMATATU AGOSTI 19,2019

Mabingwa wa Ufaransa PSG wamefanya mazungumzo na Juventus kuhusu uhamisho wa dau la £73m kumsajili mshambuliaji wa Argentina mwenye umri wa miaka 25 Paulo Dybala. (Mail)

Kiungo wa kati wa Barcelona Philippe Coutinho amewasili nchini Ujerumani ili kukamilisha mkopo wake wa msimu huu kwa mabingwa wa ujerumani Bayern Munich. (Sun)

Paris St-Germain wamemtaka beki wa Real Madrid na Ufaransa Raphael Varane, 26, pamoja na mshambuliaji wa Brazil Vinicius Junior, 19, katika mpango wa kubadilishana wachezaji iwapo wanamuitaji mshambuliaji wa Brazil mwenye umri wa miaka 27 Neymar. (Telefoot - in French)
Barcelona inatumai kumrudisha Neymar Nou Camp , lakini kukiwa na kifungu cha kumnunua.. (Sport - in Spanish)

Aliyekuwa mshambuliaji wa Tottenham Fernando Llorente, 34, anakaribia kujiunga na klabu ya Itali Lazio. Inter Milan, Fiorentina na Napoli pia zina hamu ya kumsaini raia huyo wa Uhispania , ambaye kwa sasa hana klabu. (Corriere Dello Sport - in Italian)

Inter Milan wanataka kumtoa kwa mkopo mshambuliaji wa timu hiyo raia wa Chile Alexis Sanchez, 30, na pia wana hamu na mshambuliaji Llorente na kiungo wa kati wa Barcelona na raia wa Chile Arturo Vidal, 32. (Gazzetta dello Sport - in Italian)
Ajenti wa Sanchez yuko nchini Uingereza kuzungumzia mkopo wake kuelekea Inter Milan. (Sky Italy, via Sky Sports)

Sanchez alikua akifanya mazoezi na United siku ya Jumapili alfajiri.. (The Sun)

Inter Milan inajaribu kuafikia makubaliano ya kumnunua Sanchez lakini United imelazimika kumtoa kwa mkopo ili kutolipa mshahara wake wa £500,000 kwa wiki. (Mirror)
Manchester United wanatarajiwa kuanza mazungumzo ya kumuongezea kandarasi beki Eric Bailey mchezaji mwenye umri wa miaka 25 raia wa Ivory Coast . (Sun)

Paris St-Germain na Bayern Munich huenda zikawasilisha ombi kumnunua kiungo wa kati wa Ujerumani Emre Can, 25, baada ya kuambiwa na mkufunzi wake Maurizio Sarri anahitajiki Juventus. (Tuttosport, via Mail)

Paris St-Germain na Monaco zinafikiria kumpatia ofa kiungo wa kati wa Ufaransa Tiemoue Bakayoko, 25, kwa kuwa muda wake Chelsea unaonekana kwamba umekwisha.. (Daily Express)
Celtic imeipatia ofa Bordeaux kumnunua kiungo wa kati wa Ufaransa Olivier Ntcham . (20 Minutes via Daily Record)

Mkufunzi wa Newcastle Steve Bruce yuko tayari kumrudisha uwanjani mshambuliaji wa England Dwight Gayle, 28, haraka iwezekanavyo. (Newcastle Chronicle)
Jadon Sancho anatarajiwa kuondoka Borussia Dortmund msimu ujao huku klabu hiyo ya Ujerumani ikimtafuta mchezaji atakayechukua mahala pake. (Mail)

Mkufunzi wa Crystal Palace Roy Hodgson anasema kwamba winga wa Ivory Coast Wilfried Zaha, 26, huenda akaondoka katika klabu hiyo msimu huu . (Sun)

Mshambuliaji wa Manchester United na Chile Alexis Sanchez, 30, amekataa uhamisho wa kuelekea Roma, licha ya klabu hiyo ya Old Traford kukubali kulipa kitita kikubwa cha mshahara wake wa £560k kwa wiki.{Mirror)
Hata hivyo Sanchez huenda akaelekea katika ligi ya serie A baada ya Man United kumruhusu kufanya mazungumzo na Inter Milan, ambapo huenda akakubali kupunguza mshahara wake. (Mail)

Liverpool huenda ikafaidika na £18m iwapo mshambuliaji wa zamani wa klabu hiyo na raia wa Brazil Philippe Coutinho, 27, ataelekea Bayern Munich kwa mkopo. (Mail)
Everton imetoa ofa ya kumsaini winga wa Ufaransa Franck Ribery, 36, ambaye yupo huru baada ya kuondoka Bayern Munich baada ya kuhudumu kwa miaka 12 katika klabu hiyo ambayo ndio mabingwa wa ligi ya Bundesliga . (90Min)

Kwengineko, kiungo wa kati wa Portugal Renato Sanches, 21, anataka kuondoka Bayern kwa kukosa muda wa kucheza katika klabu hiyo. (Sport1 - in German)
Mesut Ozil, 30, huenda akaondoka Arsenal na kujiunga na klabu ya DC United iwapo klabu hiyo ya ligi ya MLS inaweza kumshawishi kiungo huyo wa Ujerumani kuhamia Washington. (Star)

Beki wa kulia wa Ivory Coast Serge Aurier, 26, huenda akaondoka Tottenham na kuelekea AC Milan iwapo beki wa timu hiyo Andrea Conti, 25, ataondoka ligi ya Serie A kabla ya kukamilika kwa dirisha la uhamisho la Ulaya. (Calciomercato)

Na mchezaji wa Everton Yannick Bolasie, 30, yuko tayari kurudi katika uwanja wa Goodison Park, huku klabu za Uturuki Besiktas na Trabzonspor zikiwa na hamu ya kumsajili mchezaji huyo wa Congo . (Sun)
Mchezaji wa zamani wa Manchester City na Liverpool Mario Balotelli, 29, anakaribia kujiunga na klabu ya Serie A Brescia. (Sun via La Gazzetta)

Mshambuliaji wa Paris St-Germain Neymar, 27, hakuorodheshwa katika kikosi cha timu hiyo kitakachocheza dhidi ya Rennes kutokana na jeraha na sio kwamba raia huyo wa Brazil anataka kurudi Barcelona. (AS - in Spanish)

Mshambuliaji wa Barcelona Kevin-Prince Boateng, 32, amefichua ni kwa nini Sir Alex Ferguson hakumsajili kujiunga na Manchester United mapema wakati wa kipindi chake cha mchezo. (Goal)
Mchezaji mpya wa Man United Hannibal Mejbri, ambaye aliwasili kutoka Monaco na hawezi kutia kandarasi ya mchezaji wa kulipwa hadi atakapofikisha umri wa miaka 17 January, anataka kuvaa jezi nambari saba Old Trafford. (Mirror)
Mchezaji wa kiungo cha kati wa Ufaransa Paul Pogba, mwenye umri wa miaka 26, bado ana hamu kubwa ya kutaka kuondoka Manchester United kuelekea Real Madrid msimu huu wa joto. (Marca)

Beki wa kati wa England Harry Maguire, mwenye miaka 26, amekataa pendekezo la thamani ya £278,000 kwa wiki kutoka Manchester City badala ya kujiunga na timu hasimu United. (Star)

Meneja wa United, Ole Gunnar Solskjaer amefanya mazungumzo na mchezaji wa kiungo cha kati wa Tottenham, Christian Eriksen kuhusu uwezekano wa uhamisho kuelekea Old Trafford, hatahivyo mchezaji huyo wa miaka 27alikuwa anataka kusubiria uhamisho kuelekea Uhispania. (Manchester Evening News)

Mchezaji wa kiungo cha mbele wa United na timu ya taifa ya Chile, Alexis Sanchez, aliye na umri wa miaka 30, yupo tayari kwa uhamisho kuelekea Italia , wakati Juventus, Napoli, AC Milan na Inter Milan zote zikiwania kumsajili. (Mirror)
Sanchez atashinikiza uhamisho kuondoka Old Trafford kabla ya kufungwa kwa dirisha la uhamisho Ulaya Septemba 2. (Times)

Kwa upande mwingine, United imeshindwa kupata mnunuzi wa Sanchez- anayepokea malipo ya £560,000 kwa wiki. (Mirror)

Juventus bado inatumai kumuondoa mchezaji wa kiungo cha mbele wa Argentina, Paulo Dybala, mwenye umri wa miaka 25, kabla ya muda wa mwisho wa uhamisho Ulaya - licha ya kwamba mabingwa hao wa Italia bado hawajapokea maombi thabiti kwa mchezaji huyo. (Independent)
Watch as Colombian U21 player Anderson Diaz scores a Maradona-like Wonder goal

Mkurugenzi wa michezo wa Paris St-Germain, Leonardo anasema mchezaji wa kiungo cha mbele wa Brazil, Neymar "amefanya makosa" lakini amesisitiza kuwa mchezaji huyo wa miaka 27 yupo Paris "kwa miaka mitatu". (RMC)

Kipa wa Stoke City na timu ya taifa ya England Jack Butland, aliye na miaka 26, ataomba uhamisho kujilazimisha kuwa katika mipango ya meneja wa England, Gareth Southgate kwa ajili ya mashindano ya Euro 2020. (Mail)

Timu ya Brazil Flamengo ilmejitoa katika uhamisho wa mshambuliaji Mario Balotelli baada ya mchezaji huyo wa miaka 29 kuitisha mkataba wa thamani ya £4m. (Mail)
Napoli imekubali kumsaini winga wa Mexico mwenye miaka 23 Hirving Lozano kutoka timu ya Uholanzi PSV Eindhoven. (Voetbal International)

Napoli imekataa ombi la thamani ya £82m kutoka kwa Manchester United kwa mchezaji wa miaka 28 raia wa Senegal Kalidou Koulibaly kabla ya kufungwa kwa dirisha la uhamisho England. (Corriere dello Sport, kupitia Calciomercato)

Winga wa Bournemouth Jordon Ibe anasakwa na mabingwa wa Uskotchi, Celtic. Timu ya Napoli Italia, tayari imemuulizia mchezaji huyo wa miaka 23. (Sun)
Manchester United imewapiga marufuku wachezaji kusaini kumbukumbu au autograph kwa mashabiki katika kiingilio cha uwanja wa mazoezi kutokana na masuala ya usalama.(Telegraph)

Meneja wa West Ham Manuel Pellegrini anasema alitaka kipa wa Liverpool Adrian, mwenye miaka 32, asalie katika klabu hiyo. (Mail)

Bora za siku ya Alhamisi:

Neymar alikuwa mazoezini mwenyewe siku ya Jumatano, ataendelea kufanya hivyo mpaka atakapouzwa.(Esporte Interactivo, via Mundo Deportivo - in Spanish)Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES

Kiungo mshambuliaji wa Brazil Philippe Coutinho, 27, anaweza bado kujiunga na PSG ikiwa hatakuwa sehemu ya ofa ya Neymar. (Goal)

Beki wa kati wa Manchester United Victor Lindelof, 25, anajiandaa kusaini mkataba mpya kwa ongezeko la mshahara mbali na pauni 75,000 alizokuwa akipata kwa wiki. (Aftonbladet - in Swedish)

Bayern Munich huenda wakafufua nia yao ya kumnasa winga wa Manchester City, Leroy Sane, ingawa mchezaji huyo, 23, ana jeraha la mguu, litakalo mfanya kuwa nje ya uwanja kwa miezi saba. (Bild - in German)


Mshambuliaji wa Marseille na Italia Mario Balotelli,29, anajiandaa kutia saini mkataba wa miaka mitatu na klabu ya Brescia baada ya kukataa ofa ya Flamengo ya Brazil. (Guardian)

Flamengo bado wana matumaini ya kubadili msimamo wa Balotelli, baada ya kukubali ombi lake la kumsajili kaka yake Enock kucheza katika moja kati ya timu zao nyingine (Gazzetta dello Sport - in Italian)

Winga wa klabu ya Everton Alex Iwobi, 23, amesema aliondoka Arsenal katika siku ya mwisho ya usajili kuthibitisha kuwa yeye si mchezaji anayechipukia tena. (Mirror)

Tottenham itazungumza na Christian Eriksen, 27,tena kuhusu mkataba mpya kabla kufungwa kwa dirisha la usajili barani Ulaya, tarehe 2 mwezi Septemba, baada ya Real Madrid na Juventus kuonesha nia ya kumnasa kiungo huyo.(Independent)

Mshambuliaji wa zamani wa Liverpool Daniel Sturridge, anaonekana kujiandaa kujiunga na timu ya Trabzonspor ya Uturuki kwa dili la pauni milioni 2.8 kwa kila msimu.(Goal)

Monaco imeingia kwenye kinyang'anyiro cha kuwasajili wachezaji kiungo Blaise Matuidi,32, na beki wa kati Daniele Rugani,25, kutoka Juventus. (Gazzetta dello Sport - in Italian)
Chanzo- BBC

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527