MBUNGE WA IKOLOMANI APATA AJALI

Mbunge wa Ikolomani,Bernard Shinali amepata  ajali ya barabarani siku ya Jumapili, Agosti 18,2019 asubuhi wakati akisafiri kutoka Kakamega akielekea jijini Nairobi baada ya kuhudhuria hafla ya mazishi ya mwanawe wa kiume iliyofanyika Jumamosi

Shinali alikuwa akisafiri jijini Nairobi pamoja na watu wengine wanne wa familia yake wakati gari lake liligongana na matatu, eneo la Lessos kwenye barabara ya Kapsabet -Mau Summit.

Gari hilo lilikuwa limewabeba watu wengine wanne ambao walinusurika na wanapania kuendelea na safari yao baada ya kuandikisha taarifa kwa polisi.

 Hata hivyo, mbunge huyo alithibitisha kuwa familia yake pamoja naye wako salama salimini kupitia njia ya simu.

 Mwanasiasa huyo alikumbana na ajali hiyo wakati alikuwa akielekea jijini Nairobi baada ya kuhudhuria mazishi ya mwanawe wa kiume Chris Masakah, ambaye alikufa maji siku ya Ijumaa, Julai 26, katika jimbo la Arizona, nchini Marekani. 

Masakah alikuwa akihudumu katika jeshi la Marekani kama mwanamaji. 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527