SENGERAMA ACHAGULIWA KUWA MAKAMU MWENYEKITI HALMASHAURI YA WILAYA YA SHINYANGA



Diwani wa kata ya Iselamagazi amechaguliwa  kuwa makamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga. Uchaguzi huo umefanyika Agosti 13,2019 ambapo madiwani 35 wa halmashauri walimpigia kura Sengerema .Pichani ni Isack Sengerema akiwashukuru madiwani kwa kumchagua na kumuamini tena kwa kufikisha kipindi cha miaka mitano kutumikia nafasi  hiyo sasa tangu alipochaguliwa mwaka 2015 alipopata nafasi ya udiwani akiwa mgombea pekee aliyejitokeza. Picha zote na Kareny Masasy Malunde1 blog
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Hoja Mahiba akisoma ajenda za mkutano wa baraza la madiwani la kufunga mwaka wa 2018/2019 ambapo miongoni  ajenda zilizokuwepo ni uchaguzi wa makamu mwenyekiti ikiwa Isack Sengerema alipigiwa kura na kuchaguliwa na wajumbe 35 waliopiga kura.
Madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga wakipiga kura kuchagua makamu mwenyekiti wa halmashauri hiyo
Madiwani wakiwa katika baraza la robo ya kwanza ya mwaka wakimsikiliza mwenyekiti wa halmashauri hiyo Ngassa Mboje aliyekuwa akiendesha kikao. 
Baraka Balongo aliyekuwa msimamizi wa uchaguzi wa makamu mwenyekiti na kamati mbalimbali katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga akikabidhi nyaraka alizokuwa amekabidhiwa baada ya kukamilika uchaguzi na kupatikana mshindi.
Madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga wakisikiliza hoja mbalimbali zilizokuwa zikiibuliwa ndani ya kikao hicho. 
Madiwani wakifuatilia ajenda za kikao na kuperuzi makaburasha. 
Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya Shinyanga Ngassa Mboje akifunga kikao cha baraza la madiwani baada ya kumpata makamu mwenyekiti ambaye ni Isack Sengerema na kamati ya kudumu ya fedha, kamati za uchumi,ujenzi na mazingira, kamati ya afya ,elimu na maji kamati ya maadili na kamati ya Ukimwi. 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527