SHEHENA YA MALORI YA DAWA YATUA MUHIMBILI KUWASAIDIA MAJERUHI AJALI YA MOTO MOROGORO


Bohari ya Dawa (MSD) imekabidhi dawa na vifaa tiba kwa Hospitali ya Taifa Muhimbili, kwa ajili ya kuwahudumia majeruhi wa ajali ya moto waliohamishiwa hospitalini hapo kutoka mkoani Morogoro baada ya Kutokea kwa mlipuko wa mafuta Msamnvu Morogoro. 



Makabidhiano haya ya dawa ni mwitikio wa maombi ya dharura yaliyoombwa na Hospitali Muhimbili kwa ajili na majeruhi hao.

Meneja wa MSD, Kanda ya Dar es Salaam Bw. Celestine Haule amesema mpaka sasa jumla ya shehena ya malori matano yameshakabidhiwa Muhimbili zikiwemo dawa muhimu zinazotumika kwa ajili ya kuokoa maisha ya majeruhi hao.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527