MKURUGENZI ATCL ATOA UFAFANUZI BOMBARDIER ILIYOHARIBIKA


Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), limesema ndege aina Bombardier Q400 iliyokuwa katika matengenezo imeanza kufanya safari zake kama kawaida.


Taarifa hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), Ladslaus Matindi  leo Jumatano Agosti  21, 2019 katika kipindi cha Power Breakfast cha Redio Clouds  


Katika maelezo yake Matindi amesema ndege hiyo ilikuwa na hitilafu na ilitengenezwa kwa siku moja na tayari imerejea katika ratiba zake za safari za kila siku.

“Ndege inaweza kuharibika, kupata hitilafu au kuingiliwa na kitu kutoka nje muda wowote kwakuwa ni mashine hakuna namna ya kuzuia, hilo ni jambo la kawaida kwa mashine hata binadamu,” amesema Matindi.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527